Kamwelwe: Serikali haijasitisha ujenzi wa bandari ya Bagamoyo

May 13, 2019 3:04 pm · Nuzulack Dausen
Share
Tweet
Copy Link

Ujenzi wa mradi huo umekuwa ukipigwa kalenda mwaka hadi mwaka kutokana na kuendelea kwa majadiliano na wawekezaji. Picha|Mtandao.


  • Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Isack Kamwelwe amesema mradi huo haujasitishwa bali majadiliano yanaendelea na wawekezaji.
  • Amesema ni kweli majadiliano yamechelewa kutokana na kuwepo masharti ambayo hayana manufaa kwa upande wa Tanzania.

Dar es Salaam. Baada ya kuwepo mjadala mzito bungeni juu ya hatma ya Bandari ya Bagamoyo, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Isack Kamwelwe amesema mradi huo haujasitishwa na majadiliano yanaendelea na wawekezaji baada ya “kuwepo masharti yasiyokuwa na maslahi kwa Taifa”.

Akijibu hoja za wabunge wakati akihitimisha mjadala wa bajeti ya wizara yake, Kamwelwe amesema hadi sasa Serikali inaendelea na mazungumzo na wawekezaji wa mradi huo unaotarajia kugharimu Dola za Marekani bilioni 10 sawa na Sh22.3 trilioni.

“Kuna baadhi ya wabunge walisema Serikali imekataa kuendelea na mradi sina taarifa hiyo…majadiliano yanaendelea ila ni kweli yamechelewa kutokana na kuwepo masharti ambayo hayana manufaa kwa upande wa Tanzania,” amesema waziri huyo bila kuanisha masharti hayo.

“Pale itakapofikia ukomo wa majadiliano, Serikali itatoa taarifa kwa Bunge ili na wabunge nao watoe mchango wao,” ameongeza wakati akiomba wabunge wapitishe bajeti ya wizara hiyo ya takriban Sh5 trilioni.


Soma zaidi: Bunge lahoji kutojenga bandari ya Bagamoyo


Ujenzi wa mradi huo umekuwa ukipigwa kalenda mwaka hadi mwaka kutokana na kuendelea kwa majadiliano na wawekezaji.

Mwishoni mwaka 2017 Serikali ilieeleza kuwa ujenzi wa mradi huenda ungeanza Januari 2018 na kukamilika 2022 lakini hadi sasa bado haujaanza.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV