Kicheko kwa wafanyabiashara wanaopata TIN kwa mara ya kwanza

June 14, 2019 9:48 am · Daniel
Share
Tweet
Copy Link
  • Serikali inapendekeza kutoa unafuu wa kutolipa kodi kwa kipindi cha miezi sita kuanzia wakati mfanyabiashara au mwekezaji anapopewa Namba ya Utambulisho wa Mlipakodi (TIN).
  • Itaondoa usumbufu au dhana ya woga wakati wa kuanzisha biashara.

Dar es Salaam. Kama unakusudia kuanzisha biashara katika siku za hivi karibuni na umekuwa ukihofia kuanza kukatwa kodi wakati biashara yako ikiwa changa, sasa una kila sababu ya kutabasamu, baada ya Serikali kutoa ahueni ya kodi. 

Serikali imetangaza kusudio la kutoa nafuu ya kutolipa kodi kwa kipindi cha miezi sita kuanzia wakati mfanyabiashara au mwekezaji anapopewa Namba ya Utambulisho wa Mlipakodi (TIN). 

Akizungumza jana bungeni wakati akiwasilisha bajeti ya Serikali Kuu kwa mwaka 2019/2020,  Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango amesema hatua hii inatofautiana na hali ilivyo sasa ambapo mfanyabiashara anapopewa TIN anaanza kufanyiwa tathmini (tax assessment) ya mapato yake ya biashara na kutakiwa kulipa kodi. 

“Hatua hii itawezesha wafanyabiashara na wawekezaji wapya kupata muda wa kujiandaa na mahitaji yanayotakiwa katika shughuli wanazofanya na kuondoa usumbufu au dhana ya woga wakati wa kuanzisha biashara,” amesema Waziri Mpango. 

Amesema katika kipindi hicho mfanyabiashara anakuwa anashughulikia  mahitaji ya Leseni ya biashara na vibali vingine muhimu vya biashara, jambo litakamsaidia kujipanga kabla hajaanza kulipa kodi.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
21 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
21 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
21 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwanzo mwisho mapokezi ya Rais wa Namibia Netumbo Nandi Ikulu Dar es Salaam

Mwanzo mwisho mapokezi ya Rais wa Namibia Netumbo Nandi Ikulu Dar es Salaam

Nukta TV

Sikia kisa cha bibi wa Mbagala, chanzo Jaji Mkuu Masaju kupanda cheo

Sikia kisa cha bibi wa Mbagala, chanzo Jaji Mkuu Masaju kupanda cheo

Nukta TV

FAHAMU KUHUSU SIKOSELI | Part 1: Ugonjwa wa kurithi, unaotesa maelfu ya watoto Tanzania

FAHAMU KUHUSU SIKOSELI | Part 1: Ugonjwa wa kurithi, unaotesa maelfu ya watoto Tanzania

Nukta TV