Tanzania yapewa jukumu la kuongoza kamati ya hali ya hewa SADC

August 14, 2019 2:01 pm · Rodgers Raphael
Share
Tweet
Copy Link
  • Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) Dk Agnes Kijazi ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa kamati hiyo. 
  • Ataongoza kamati hiyo kwa kipindi cha miaka miwili. 

Dar es Salaam. Tanzania amekabidhiwa uenyekiti wa kamati ndogo ya sekta ya hali ya hewa ya Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) kwa kipindi cha miaka miwili, jambo linalofungua fursa za kufaidika zaidi na huduma za hali ya hewa katika jumuiya hiyo.  

Makabidhiano hayo yamefanyika katika mkutano wa kamati hiyo (SADC-SCOM) jijini Windhoek, Namibia Agosti 13, 2019 ambapo Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) Dk Agnes Kijazi ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa kamati hiyo. 

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na TMA, Dk Kijazi amepita bila kupingwa na atashikilia nafasi hiyo kwa kipindi cha miaka miwili kuanzia mwaka huu wa  2019.

Dk Kijazi anachukua nafasi ya Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Hali ya Hewa ya Namibia, Franz Uirab ambaye ameiongoza kamati hiyo kwa miaka miwili. 

Sambamba na makabidhiano hayo, mkutano huo umejadili masuala mbalimbali ya uendelezaji wa sekta ya hali ya hewa katika eneo la SADC pamoja na kupitia hatua za utekelezaji wa maamuzi ya mkutano wa Mawaziri uliopita na kutoa mapendekezo yatakayjadiliwa Septemba, 2019 Jijini Dar es Salaam.

/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
25 May, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
25 May, 2026
No active movers today
Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
MIKOA 5 YA KIPOLISI INAYOONGOZA KWA MAKOSA BARABARANI

MIKOA 5 YA KIPOLISI INAYOONGOZA KWA MAKOSA BARABARANI

Nukta TV

SERIKALI YAKAMILISHA MAZUNGUMZO MRADI WA LIGANGA NA MCHUCHUMA

SERIKALI YAKAMILISHA MAZUNGUMZO MRADI WA LIGANGA NA MCHUCHUMA

Nukta TV

🔴LIVE: KAPINGA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA 2026/2027 BUNGENI.

🔴LIVE: KAPINGA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA 2026/2027 BUNGENI.

Nukta TV