Facebook yawarahisishia maisha wapenzi wa filamu

August 16, 2019 1:42 pm · TULINAGWE ALSON
Share
Tweet
Copy Link
  • Inakusudia kuwawekea kipengele cha kupata taarifa za filamu wanazozipenda kwa urahisi na haraka.
  • Pia itawawezesha kupata tiketi na kufahamu kumbi za sinema zinazoonyesha filamu husika. 

Katika kuwafikia na kukidhi mahitaji ya watumiaji wake, Facebook iko mbioni kuanzisha kipengele kipya kitakachowarahisishia wapenzi wa filamu kupata kwa haraka risiti zinazowawezesha kuingia katika kumbi za sinema. 

Kipengele hicho kinatarajiwa kuanza kutumika hivi karibuni ambapo mpenzi wa filamu ataweza kutafuta filamu anazizopenda na kujulishwa pale filamu hiyo inapokua imetoka kwajili ya kutazamwa.

Mteja atatakiwa kuingia katika ukurasa wake wa juu (News feed) na kuchagua filamu anayoipenda na kubonyeza kitufe cha  ‘Interested’ CTA button’ kitakachomwezesha kupata taarifa zote pindi filamu hiyo inapokua iko tayari.


Zinazohusiana


Mabadiliko mengine ni pamoja na mtumiaji ataweza kutafuta filamu anayopenda katika “Search Engine” na kupata taarifa za kina kuhusu filamu hiyo ikiwemo namna ya kupata tiketi na ukumbi anaoweza kuipata filamu hiyo.

Mabadiliko haya yataleta urahisi kwa wapenzi wa filamu kujua ni filamu gani zimetoka karibuni na kufuata taratibu zote zinazotakiwa kufanyika kwa urahisi bila kupata shida yoyote kama ambavyo mtu angekua akifanya bila ya maboresho hayo kufanyika hapo awali.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
25 Aug, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
25 Aug, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
25 Aug, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Elimu ya kodi mwarobaini wa wafanyabiashara kuikwepa TRA, ianzie shuleni

Elimu ya kodi mwarobaini wa wafanyabiashara kuikwepa TRA, ianzie shuleni

Nukta TV

Rais Samia: Serikali chini ya Magufuli haikutaka kuyumbishwa kukamili kwa JNHPP

Rais Samia: Serikali chini ya Magufuli haikutaka kuyumbishwa kukamili kwa JNHPP

Nukta TV

Rais Samia: Umeme wa SGR hautoingiliwa, Dodoma umeme uhakika 24/7

Rais Samia: Umeme wa SGR hautoingiliwa, Dodoma umeme uhakika 24/7

Nukta TV