Heslb yatakiwa kutoa mikopo kwa wanafunzi waliosomeshwa kwa ufadhili

September 23, 2019 7:38 am · Rodgers Raphael
Share
Tweet
Copy Link
  • Aitaka Bodi ya mikipo kuwapa mikopo wanafunzi wote ambao walikua wakisoma shule binafsi kwa ufadhili.
  • Amewataka wanafunzi hao kuwasiliana na Bodi ili waweze kusaidiwa.
  • Agizo kama hilo alilitoa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa Agosti 10, 2019.

Dar es Salaam. Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako, ameitaka Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) kuwapa mikopo wanafunzi wote ambao walikua wakisoma shule binafsi kwa ufadhili.

Waziri huyo amesema kumejengeka dhana ya wanafunzi wanaosoma shule binafsi hawana uhitaji wa kupata mikopo kwa sababu wazazi au walezi wana uwezo wa kuwasomesha. 

Prof. Ndalichako ametofautiana na dhana hiyo na kusema siyo sahihi kwani wapo wanafunzi wanaosomeshwa na watu binafsi au wadhamini mbalimbali zikiwemo taasisi za kidini. 

“Naomba niwahakikishie kuwa Serikali inatambua watoto hawa ambao wanasomeshwa katika shule binafsi hivyo wanapojiunga na elimu ya juu watapatiwa mikopo ila wanatakiwa kuzingatia kujaza maelezo yao vizuri kwenye fomu ya mikopo,” amesema Prof. Ndalichako.


Zinazohusiana


Ametoa agizo hilo jana (Septemba 22, 2019) jijini Dar es Salaam, wakati akifungua wiki ya elimu na kituo cha kulelea watoto wanye uhitaji katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKKT), usharika wa Kimara.

Katika kuhakikisha wanafunzi hao hawapishani na fursa hiyo, amewataka wanafunzi ambao walikuwa wamewasilisha fomu za maombi ya mikopo bila kujaza taarifa za ufadhili kuwasiliana na bodi hiyo ili waweze kuongezea taarifa hizo.

“Kama wapo ambao walishindwa kujaza vyema maelezo yao, bodi bado inaendelea na usajili ni muhimu wakaenda kuomba kufanya marekebisho wajaze taarifa hizo kwa usahihi ili waweze kunufaika na mikopo,” amesema.

Agizo kama hilo liliwahi kutolewa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa zaidi ya mwezi mmoja uliopita ambapo aliitaka Bodi hiyo kutafakari utoaji wa mikopo kwa wanafunzi waliosoma shule binafsi.

Majaliwa alisema wapo wanafunzi wanaofaulu vizuri kidato cha nne na kukosa nafasi katika shule za Serikali na kutokana na kutoka katika familia zisizokuwa na uwezo, wengi wao hutafuta wafadhili na kusoma kwenye shule binafsi.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV