Ndiyo! mama aliyeambukizwa Corona anaweza kumnyonyesha mtoto wake
- Anashauriwa kuchukua tahadhari zilizoainishwa ikiwa ni pamoja na kuvaa barakoa na kunawa mikono.
- Pia, sehemu ambazo mama huyo amezishika, zinatakiwa kusafishwa mara kwa mara kwa kutumia vitakasa (sanitizers).
Dar es Salaam. Ugonjwa wa corona umeibua sintofahamu nyingi na kufanya watu kuhoji kama kila wanachokifanya hakitawaweka wao au wale wawapendao kwenye hatari ya kuambukizwa ugonjwa huo aina ya COVID-19.
Kati ya sintofahamu hizo ni ya mama anayenyonyesha kama anaweza kufanya hivyo pale anapogundulika kuwa ana COVID-19.
Shirika la Afya Duniani (WHO) limesema hadi sasa hakuna utafiti unaoonyesha kuwa maziwa kutoka kwa mama mwenye COVID-19 yanaweza kumuambukiza mtoto pale anaponyonya maziwa hayo.
Zinazohusiana
- Utapigwa: Hakuna mabilioni ya msaada wa corona yanatolewa na akaunti ya Facebook
- Corona yachangia wanafunzi 4,000 kupata mimba Kenya
“Hakuna sababu ya kuepuka au kuacha kunyonyesha,” imeeleza WHO.
Hata hivyo, WHO imesema ili kujiweka salama, mama anayenyonyesha anakiwa kuchukua tahadhari muhimu za kumkinga mtoto wake dhidi ya ugonjwa huo ikiwemo kunawa mikono na maji tiririka na sabuni mara kwa mara kabla na baada ya kumnyonyesha mtoto.
Pia, mama anatakiwa kuvaa barakoa pale anapokuwa ananyonyesha na kutumia tishu anapopiga chafya na kuzitupa mahali salama.
Pamoja na hayo, sehemu zote ambazo mama huyo anakuwa amezishika, zisafishwe mara kwa mara kwa kutumia vitakasa (sanitizers).
Latest
