Video: Utarajie nini unapozeeka?

September 1, 2020 3:03 am · Rodgers Raphael
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni pamoja na maungio ya mwili kuchoka huku baadhi yao wakikosa usingizi.
  • Wazee wanashauriwa kutumia vyakula vyenye vitamini zaidi na kufanya mazoezi.

Dar es Salaam. Bila shaka ungependa kubaki na mwili wa ujana kwa muda mrefu lakini jambo hilo haliwezekani kwa sababu miili yetu imeumbwa kuchakaa kadiri unavyopitia mabadiliko mbalimbali kuelekea uzeeni.

Kitaalamu, mbadiliko hayo huitwa “degenerative changes” ambayo kwa mujibu wa wataalamu wa afya, yanaambatana na changamoto nyingi zikiwemo kukosa usingizi na kufifia kwa uimara wa maungio ya mwili. 

Mfiziotherapia Dk Joshua Sultan ameiambia Nukta Habari (www.nukta.co.tz) kuwa unaweza kupunguza makali yanayoambatana na uzee kwa kufanya mazoezi, kula vyakula vinavyofaa na kujitahidi kupunguza uzito.

Je, ni mabadiliko yapi yanayoambatana na uzee? Tazama video hii #NuktaVideoYaSiku

Follow Us on TikTok

FOLLOW NOW

Subscribe to Our YouTube Channel

SUBSCRIBE NOW