Video: Umuhimu wa kufanya utafiti wa masoko kabla ya kuanza biashara

September 18, 2020 1:31 pm · Rodgers Raphael
Share
Tweet
Copy Link
  • Kufanya utafiti itakusaidia kufahamu kama kweli bidhaa yako inahitajika sokoni.
  • Pia itakusaidia kuwafahamu washindani wako pamoja na kulielewa soko lenyewe.
  • Kwa upande wa hasara, itakuepusha kuwekeza mamilioni kwenye biashara ambayo haina faida.

Dar es Salaam. Kabla ya kuanza biashara yoyote, hautakiwi kukurupuka. Inakuhitaji kuwa na mipango madhubuti ili kuepuka majuto baada ya fedha ulizowekeza kupotea bure.

Kati ya mipango muhimu ya kuzingatia ni pamoja na kufanya utafiti wa masoko kabla ya kujiingiza kwenye biashara mzima mzima.

Utafiti wa kimasoko ni kitendo kinachodhamiria kufahamu mambo mbalimbali kuhusu soko la bidhaa au huduma na mahitaji ya watumiaji wa bidhaa husika.

Mbali na kukusaidia kuwa mbunifu kwenye bidhaa yako baada ya kufahamu madhaifu ya bidhaa zilizopo sokoni zinazoshabiiana na yako, utafiti utakusaidia kuepuka hasara zinazoweza kujitokeza endapo utajiingiza kwenye biashara bila kufanya utafiti.

Pia, itakusaidia kuwafahamu washindani wako na hivyo kukufanya uwe mbunifu ili uweze kushindana nao sokoni.

Unataka kujua wataalamu wa masoko wanasemaje, tazama video hii.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Rais Samia azindua minara 758, aacha maagizo mazito juu ya mkongo wa taifa

Rais Samia azindua minara 758, aacha maagizo mazito juu ya mkongo wa taifa

Nukta TV

JAJI MKUU: Njia za asili ni mojawapo ya njia halali za utatuzi wa migogoro

JAJI MKUU: Njia za asili ni mojawapo ya njia halali za utatuzi wa migogoro

Nukta TV

Hesabu ya bosi, bei ya mafuta pasua kichwa madereva wa daladala

Hesabu ya bosi, bei ya mafuta pasua kichwa madereva wa daladala

Nukta TV