Jinsi ya kukabiliana na tatizo la kuharibika kwa mimba

November 23, 2020 12:58 pm · Rodgers Raphael
Share
Tweet
Copy Link
  • Tatizo hilo husababishwa na mambo mengi ikiwemo uzito uliopitilizwa ama mjamzito kupigwa tumboni.
  • Pia, uvimbe kwenye kizazi huweza kuwa sababu ya baadhi ya wanawake kukubana na changamoto hiyo.
  • Baada ya kukumbana na tatizo hilo, mtu anashauriwa kutumia dawa kwa kuzingatia maelezo aliyopewa na mtoa huduma za afya.

Dar es Salaam. Kupata watoto baada ya kuingia kwenye ndoa ni moja ya malengo ya wanandoa wengi wengi. 

Lakini suala la kupata mtoto huusisha mchakato mrefu ambao unahitaji umakini hasa kwa mama mjamzito ili kuepusha mimba kuharibika na hatimaye kutoka kabla ya wakati. 

Kuharibika kwa ujauzito husababishwa na vitu mbalimbali ikiwemo matatizo katika maumbile ya mfuko wa uzazi. 

Kwa mujibu wa tovuti ya afya ya Tanzmend, mimba huharibika kutokana na kutokuwepo kwa uwiano wa vichocheo (hormonal inbalance) hasa upungufu wa kichocheo aina ya “progesterone” ambacho ni muhimu sana katika ukuaji wa mimba.

Sababu zingine ni pamoja na uvimbe kwenye kizazi, kulegea kwa shingo ya kizazi, mjamzito kuwa na kinga ya mwili dhaifu, kufanya kazi ngumu na kwa muda mrefu, kupigwa kwa mjamzito kwenye tumbo, utapiamlo na uzito uliopitiliza.

Dalili za kuharibika kwa mimba

Tanzmed imeainisha kuwa “kutokwa damu kwenye sehemu za siri za mwanamke ambapo huanza kama matone na baadaye kuongezeka kuwa nyingi, maumivu ya tumbo chini ya kitovu, homa na ulegevu pamoja na maumivu ya kiuno.”

Ufanye nini endapo hali hiyo imekukuta? Tazama video hii kujifunza zaidi:

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
26 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
27 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
27 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Hizi ndio passport 5 zenye nguvu zaidi duniani

Hizi ndio passport 5 zenye nguvu zaidi duniani

Nukta TV

Hii ndio spirulina: Hazina ya maji inayoboresha afya za Watanzania

Hii ndio spirulina: Hazina ya maji inayoboresha afya za Watanzania

Nukta TV

Mradi wa Sh4.6 bilioni kutoa ahueni ya umeme Lindi, Mtwara

Mradi wa Sh4.6 bilioni kutoa ahueni ya umeme Lindi, Mtwara

Nukta TV