Tasaf kuziinua kaya masikini zaidi ya 5,000 Tanzania

February 4, 2021 11:59 am · Mariam John
Share
Tweet
Copy Link
  • Zitaingizwa katika Mpango wa Taifa wa Kunusuru Kaya Masikini (Tasaf) ili ziweze kujikwamua kiuchumi.
  • Ni zile ambazo hazikuwahi kupitiwa na mpango huo tangu awamu ya kwanza ilipoanza.

Mwanza. Serikali ipo mbioni kuziingiza zaidi ya kaya 5,500 za Tanzania kwenye Mpango wa Taifa wa Kunusuru Kaya Masikini (Tasaf) ili ziweze kujikwamua kiuchumi.

Kaya hizo zitakazoingizwa kwenye mpango huo ni zile ambazo hazikuwahi kupitiwa na mpango huo tangu awamu ya kwanza ilipoanza.

Mkurugenzi wa mawasiliano  Tasaf Taifa, Zuhura Mdungi akizungumza baada ya kutembelea na kukagua maendeleo ya walengwa katika Wilaya za Magu na Misungwi mkoani Mwanza, amesema mpaka sasa zoezi la kuwatambua walengwa hao limeshakamilika na utaratibu wa kuwaingiza kwenye mpango utafanyika hivi karibuni.

“Tumefanya tathmini na tayari taratibu za kuwaingiza zitaanza hivi karibuni,”amesema Mdungi jana Februari 3 akiwa Mwanza.

Akiwa ameambatana na timu ya wataalam Tasaf Taifa, Mratibu wa mpango huo wilayani Magu, Daniel Sanyege ameeleza kuwa wilaya hiyo ina zaidi ya walengwa 4,998 ambao wengi wao wamenufaika na fedha hizo kwa kukuza uchumi wa familia zao. 

Katika wilaya ya Magu pekee zaidi ya Sh3 bilioni zimetumika katika kipindi cha miaka sita kuzinusuru  kaya masikini wilayani humo. 


Soma zaidi: 


Magu ilivyofaidika na fedha za Tasaf

Sanyenge anaeleza kuwa ruzuku inayotolewa na Tasaf imesaidia kaya nyingi masikini kuweza kupeleka watoto wao shule jambo ambalo limesaidia watoto wengi kufika ngazi ya chuo kikuu.

“Tuna watoto sita wanaotokea kaya masikini wanaendelea na masomo ya vyuo vikuu, watoto wengine 27 wanasoma elimu ya sekondari kidato cha tano na sita, haya ni mafanikio makubwa ambayo bila kuwezeshwa watoto hao wasingetimiza ndoto zao,” amesema Sanyenge

Mafanikio mengine ambayo walengwa wamefanikiwa ni pamoja na kujenga nyumba za bati, kununuaa ng’ombe pamoja na kufanya miradi ya maendeleo.

“ Kabla sijaingizwa kwenye mpango huu nilikuwa nalala njaa, kwa sasa naishukru Tasaf kwa kuwa imenisaidia nimejenge nyumba na ninafanya ufugaji,”amesema Makoye Linda mkazi wa Nyashiwa wilayani humo.

Mbali na mafanikio hayo,  Tasaf pia imefanikisha kujenga visima vya maji 150 kwa ajili ya matumizi ya nyumbani, pia wamefanikiwa kuchimba malambo 32 kwa ajili ya kunyweshea mifugo, kufulia na kufanyia ujenzi.

Mkazi wa kijiji cha Nyanag’omango wilayani Misungwi, Benedatha Shija anasema kabla ya mradi huo walilazimika kutembea umbali wa kilomita 10 kufuata maji.

“Taunaishukru Serikali kupitia Tasaf kwa kutujengea miradi ya maji ambayo tunatumia kwa matumizi  ya nyumbani,” amesema Shija. 

/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
5 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
5 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Wabunge waliokwenda Morocco bila kibali kikaangoni , utoro ukiibuliwa bungeni

Wabunge waliokwenda Morocco bila kibali kikaangoni , utoro ukiibuliwa bungeni

Nukta TV

Mfahamu Leonard Mususa Alama ya Ungozi iliyoacha majonzi kwa 'MACEOs' Tanzania

Mfahamu Leonard Mususa Alama ya Ungozi iliyoacha majonzi kwa 'MACEOs' Tanzania

Nukta TV

Bei za mafuta mwezi Juni hizi hapa, dizeli ikipaa kwa Sh85

Bei za mafuta mwezi Juni hizi hapa, dizeli ikipaa kwa Sh85

Nukta TV