Kigogo TPA aliyesimamishwa kazi na Rais Samia mikononi mwa Takukuru

March 30, 2021 7:55 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Takukuru yasema hajatoroka bali wanamshikilia kwa mahojiano na uchunguzi. 
  • Alisimamishwa kazi na Rais Samia Suluhu Hassan Machi 28 baada ya kubainika uwepo wa ubadhirifu wa Sh3.6 bilioni bandarini.

Dar es Salaam. Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Deusdedit Kakoko aliyesimamishwa kazi wiki iliyopita ili kupisha uchunguzi wa ubadhirifu dhidi ya taasisi hiyo, sasa anashikiliwa na kuhojiwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania (Takukuru). 

Takukuru imesema bosi huyo wa TPA hajatoroka kama inavyodaiwa na baadhi ya watu mtandaoni  bali inamshikilia kwa uchunguzi. 

Rais Samia Suluhu Hassan alimsimamisha kazi Kakoko Machi 28 mwaka huu baada ya kubainika uwepo wa ubadhirifu wa Sh3.6 bilioni bandarini. 

“Wakati Waziri Mkuu amefanya ukaguzi waliosimamishwa ni hawa wa chini huku naomba mara moja nitoe agizo la kumsimamisha mkurugenzi mkuu wa bandari. Halafu uchunguzi uendelee,” aliagiza Rais Samia wakati akipokea ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kwa mwaka 2019/20 Ikulu jijini Dodoma. 


Soma zaidi:


Hata hivyo, Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, Brigedia Generali John Mbungo amejitokeza na kusema hajatoroka bali wanamshikilia bosi huyo wa TPA kwa ajili ya uchunguzi. 

“Kumshikilia mtu ni suala la kawaida kama kuna tatizo limetokea na kama mlivyomsikia Mheshimiwa Rais amemsimamisha kazi kwa sababu ya matatizo na sisi ni kweli tunamshikilia ili tuweze kufanya uchunguzi vizuri”- Brigedia Jenerali Mbungo wakati akihojiwa na kituo cha televisheni cha ITV leo Machi 30,2021. 

Hata hivyo, Mkurugenzi mkuu huyo wa Takukuru amesema kwa sasa hawezi kusema kuhusu sababu za kumshikilia bosi huyo lakini ni utaratibu wa uchunguzi. 

Kakoko, ambaye alithibitishwa kuwa bosi wa TPA mwaka 2018 baada ya kuwa kaimu wa taasisi hiyo, anakuwa kiongozi wa awali kabisa kusimamishwa kazi na Rais Samia ambaye alitwaa madaraka Machi 19 mwaka huu baada ya kufariki kwa aliyekuwa Rais wa Tanzania Dk John Magufuli. 

/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
5 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
5 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Wabunge waliokwenda Morocco bila kibali kikaangoni , utoro ukiibuliwa bungeni

Wabunge waliokwenda Morocco bila kibali kikaangoni , utoro ukiibuliwa bungeni

Nukta TV

Mfahamu Leonard Mususa Alama ya Ungozi iliyoacha majonzi kwa 'MACEOs' Tanzania

Mfahamu Leonard Mususa Alama ya Ungozi iliyoacha majonzi kwa 'MACEOs' Tanzania

Nukta TV

Bei za mafuta mwezi Juni hizi hapa, dizeli ikipaa kwa Sh85

Bei za mafuta mwezi Juni hizi hapa, dizeli ikipaa kwa Sh85

Nukta TV