Ziara ya Rais Magufuli Ruvuma yamng’oa kigogo wa halmashauri

April 9, 2019 11:19 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma, Dk Oscar Mbyuzi aliyefutwa kazi na Rais Magufuli leo. Picha|Mtandao.


  • Ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma, Dk Oscar Mbyuzi ambaye uteuzi wake umetenguliwa leo na nafasi yake imechukuliwa na Jimson Mhagama.
  • Sababu za kutenguliwa kwa Mmkurugenzi huyo bado hazijatajwa.

Dar es Salaam. Rais John Magufuli leo ametengua uteuzi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma, Dk Oscar Mbyuzi.

Taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu leo (Aprili 9, 2019) inaeleza kuwa kufuatia uamuzi huo, Rais Magufuli amemteua Jimson Mhagama kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo ambapo uteuzi wa Mhagama unaanza mara moja.

Hata hivyo, taarifa hiyo haijaweka bayana sababu za kigogo huyo kutolewa katika nafasi hiyo.

Mabadiliko hayo ya uongozi yanakuja wakati Rais Magufuli akikamilisha ziara ya siku sita mkoani Ruvuma aliyoanza tangu Aprili 4 mwaka huu ambapo leo anazindua kituo cha afya cha Madaba kilichopo Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.

Akiwa mkoani humo, Rais ametumia muda wake mwingi kuwaonya viongozi wa Serikali wakiwemo wakuu wa wilaya kutimiza majukumu yao kikamilifu na kuhakikisha wanawatumikia wananchi kwa kuwaondolea shida zao ikiwemo kuboresha huduma za kijamii.  

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
25 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
25 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
25 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Hizi ndio passport 5 zenye nguvu zaidi duniani

Hizi ndio passport 5 zenye nguvu zaidi duniani

Nukta TV

Hii ndio spirulina: Hazina ya maji inayoboresha afya za Watanzania

Hii ndio spirulina: Hazina ya maji inayoboresha afya za Watanzania

Nukta TV

Mradi wa Sh4.6 bilioni kutoa ahueni ya umeme Lindi, Mtwara

Mradi wa Sh4.6 bilioni kutoa ahueni ya umeme Lindi, Mtwara

Nukta TV