Wamarekani waunda kifaa cha kuwasaidia wanaokoroma usingizini

October 23, 2019 2:33 pm · TULINAGWE ALSON
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni kifaa chenye kusaidia mfumo wa upumuaji mtu akiwa kwenye usingizi mzito.
  • Umuhimu wa kifaa hicho kinasaidia mtu kupumua vizuri bila shida pindi anapokuwa kwenye usingizi.

Dar es Salaam. Usingizi ni kitu chenye kuleta afya kwa kila binadamu anaeishi ila namna tunavyolala inatofautiana kulingana na tunavyoweza kuingiza na kutoa pumzi wakati wa kulala. 

Kulala kwa kukoroma kunaweza kusababishwa na ugumu wa kupumua kipindi mtu anapokuwa usingizini au matatizo katika mfumo wa kupumulia katika pua za mtu na kumsababishia kuwa na desturi ya kukoroma pindi anapokuwa kwenye usingizi mzito.

Hali hii huwa kero pale mtu anapokuwa jirani na mwenzie na kusikika akikoroma anapokuwa amelala licha ya kutokujijua kwa sababu anakuwa kwenye usingizi mzito.

Kumalizia tatizo hilo, Wamarekani wamegundua kifaa kinachoitwa Silent Snore kinachosaidia mtu anapokuwa usingizini asisikike kama anakoroma usiku mzima mpaka anapoamka kutoka usingizini.

Kifaa hicho kinafanya kazi kwa kupachikwa kwenye pande zote mbili za pua. Baada ya kukiweka puani kinasaidia mtu kuwa na uwezo mkubwa wa kupumua vizuri bila shida akiwa usingizini hata kama ana desturi ya kukoroma.

Silent Snore inasaidia kupunguza kero ya kukoroma na kuweka mdomo kwenye hali nzuri kwani inasababisha mtu kufumba mdomo pindi anapokuwa amelala kutoana na kifaa hicho kinachowekwa puani.

Kifaa hicho pia kinamweka mtu huru pindi anapokuwa amelala kujua kwamba amelala bila kusumbua watu kwa sauti za kukoroma tofauti na pale anapokuwa hajatumia kifaa hicho usingizini.

Charles Msinde, Daktari katika hospitali ya Mama Ngoma anasema kifaa hicho kinaweza kuwa na umuhimu wa kumsaidia mtu katika ulalaji wake lakini vilevile inaweza kuwa na athari kiafya kwani kinazuia upumuaji unaotakiwa.

“Hakiwezi kuwa effective (fasaha) kwa asilimia 100 kwani ukikibana kwenye pua maana yake kuna mifumo fulani inazuiliwa kutoa hewa pindi mtu anapokuwa usingizini. Hivyo si cha kukizoea sana,” amesema Msinde.

Kifaa hicho kinadaiwa kuwa ni cha kwanza kuletwa kwa ajili ya kuzuia upumuaji mgumu mtu akiwa usingizini na kinatarajia kufika Tanzania karibuni kwa matumizi kwa watu wenye uhitaji na matatizo hayo wakati wa kulala.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.