Wakulima washauriwa kutumia teknolojia ya kisasa ya kilimo cha umwagiliaji

September 18, 2018 5:35 pm · Rodgers Raphael
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni kile kinachotumia mfumo wa matone kinachopunguza upotevu wa maji na kuongeza mavuno.
  • Wakulima wengi bado wanalima kilimo cha kienyeji cha umwagiliaji.

Dar es Salaam. Licha ya watanzania wengi kuchangamkia kilimo cha umwagiliaji kama njia ya kujipatia kipato, bado wanakabiliwa na changamoto ya kulima kienyeji ikiwemo matumizi yasiyo sahihi ya maji na miundombinu duni ya umwagiliaji, jambo linalowakwamisha kufaidika na kilimo hicho.

Inakadiriwa kuwa hekta 461,000 sawa na asilimia 5 ndiyo zinatumika kwa kilimo cha umwagiliaji kati ya hekta 29.4 milioni zilizopo kutokana na kilimo cha mazoea na uwekezaji mdogo unaofanywa kwenye sekta hiyo

Hata wakulima wanaolima kienyeji bado wanakabiliwa na changamoto ya matumizi mabaya ya maji ikiwemo upotevu wa kiasi kikubwa cha maji kinachopotea kwasababu ya kukosa miundombinu ya kisasa kusimamia maji na ukuaji wa mazao.

Kutokana na changamoto hizo, kampuni ya vifaa vya umwagiliaji ya Vishakha kutoka India imekuja na teknolojia ya umwagiliaji kwa njia ya matone ambayo inaweza kuwa mkombozi kwa wakulima wa Tanzania wenye nia ya kuendeleza sekta ya umwagiliaji nchini.

Kilimo cha umwagiliaji kinaweza kuboreshwa ikiwa wakulima watapewa teknolojia ya kisasa. Picha| Wikipedia.

Mshauri wa maendeleo ya Biashara kutoka kampuni hiyo, Mayur Parikh amesema teknolojia ya matone inasaidia kuondokana na changamoto za kilimo cha mazoea cha kutumia maji mengi bila kuzingatia mahitaji ya mimea.

“Ni vyema tutumie maji kwa ufanisi katika kilimo cha umwagiliaji kwa maslahi ya kilimo,” amesema Parikh.

Tofauti na mashine zingine za umwagiliaji, mashine za Vishakha humwagilia maji kwa mfumo wa matone hasa kwa mazoa yanayolimwa kwa ukaribu kama miwa, mboga mboga, pamba, ndizi na maua kwa kuunganisha mpira wenye matundu yanayopitisha maji moja kwa moja kwenye shina la mmea.

Kwa kutumia vifaa hivyo, mkulima huweza kutumia kiasi kidogo cha maji kwa siku na hivyo kuepusha gharama za umeme kama anatumia pampu ya kurusha maji shambani. Pia anaokoa muda wa kukaa shambani kwa muda mrefu na kumpa nafasi ya kufanya shughuli zingine za uzalishaji.

Parikh anabainisha kuwa umwagiliaji wa matone unatoa uhakika wa mazao kupata maji ya kutosha na kukua kwa wakati na kumpatia mkulima mazao yanayoendana na gharama za uzalishaji.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.