Uber yatoa masharti mapya kwa madereva wake

May 18, 2020 8:08 am · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Dereva hataruhusiwa kubeba abiria mpaka awe amevaa barakoa.
  • Pia anatakiwa kuwa na kitakasa mikono na kunawa mikono mara kwa mara. 
  • Abiria nao wanatakiwa kuvaa barakoa wakati wote wa safari.

Dar es Salaam. Kampuni ya usafiri wa mtandaoni ya Uber leo imeanza kutekeleza masharti mapya yanayowataka madereva wake kujipiga picha inayoonyesha wamevaa barakoa kabla ya kuwabeba abiria ili kuzuia maambukizi ya virusi vya Corona  wakati wanatumia usafiri huo. 

Picha hiyo inatakiwa kupigwa kwa kutumia programu ya simu (App) ya Uber ambayo itathibitisha kuwa dereva anaweza kumbeba abiria. 

Uber katika taarifa yake iliyotolewa Jumatano Mei 13, 2020 imeeleza kuwa hiyo ni sehemu ya mambo muhimu ambayo dereva anatakiwa kutekeleza kabla hajatumia app hiyo kila siku.

“Kwa sasa majiji yameanza kufunguliwa tena na watu wameanza shughuli zao, Uber inaendelea kuchukua tahadhari  na kuhakikisha tunatimiza wajibu wetu kumsaidia kila mmoja kuwa salama kiafya akiwa anasafiri,” inaeleza sehemu ya taarifa ya Uber. 

Madereva wa Uber wanatakiwa kuthibitisha kuwa hawana dalili za Corona, wana vitakasa mikono (sanitizers), wanaosha mikono mara kwa mara. 

Pia, abiria wanaotumia usafiri wa Uber (taxi, bodaboda na bajaji) wanatakiwa kuthibitisha kuwa wamevaa barakoa au kifunika uso kabla ya kuita gari.


Zinazohusiana:


Wao hawatakiwi kujipiga picha (selfie) lakini Uber wamesema wanatarajia kuona madereva na abiria wanawajibishana katika kuchukua tahadhari ya kujikinga na COVID-19. 

Ikiwa dereva na abiria hawajavaa barakoa au kifunika uso, safari yao haitahesabika kwenye app ya Uber kwa sababu wataondolewa mtandaoni kwa wakati huo. 

Hata hivyo, hakutakuwa na faini ya kukiuka masharti yaliyowekwa na Uber.

Kampuni hiyo yenye makao makuu nchini Marekani imesema masharti hayo yatadumu hadi mwezi Juni kabla hayafanyiwa tathmini kulingana na mwenendo wa ugonjwa wa COVID-19. 

Aidha, Uber imesema imetenga dola za Marekani 50 milioni (Sh115.7 bilioni) kwa ajili ya kununua vifaa tiba zikiwemo barakoa, vitakasa mikono, sabuni na vifaa vya kuoshea magari kwa ajili ya madereva wake. 

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.