Tusipoteze muda na wasioamini katika mabadiliko ya tabianchi-Kabudi

September 27, 2019 1:35 pm · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Waziri huyo Mambo ya Nje ameitaka jumuiya ya kimataifa kuwajibika na  isipoteze muda na watu wasioamini katika uharibifu wa mazingira.
  • Amesema nchi zilizoendelea kiviwanda zina wajibu wa kufanya kupunguza hewa ukaa.

Dar es Salaam. Waziri wa Mambo ya Nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki,  Profesa Palamagamba John Kabudi ameitaka jumuiya ya kimataifa kuwajibika na  isipoteze muda na watu wasioamini katika uharibifu wa mazingira unaosababisha mabadiliko ya tabianchi ikiwemo ukame na ongezeko la joto. 

Prof. Kabudi amezengumzia hatua hiyo wakati akihojiwa na Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani kabla ya kuhutubia mkutano wa baraza kuu la UN na kusema kila nchi itakiwa kuwajibika kwa kuwekeza fedha ili kuokoa mazingira. 

“Wako ambao wanakana kwamba tatizo hilo halipo, hao tusipoteze muda wetu sana, lakini wale wanaokiri kwamba tatizo hilo lipo wajue kuwa wanapotoa fedha zao kwa ajili ya kutekeleza miradi ya kushughulikia tatizo hilo katika nchi zinazoendelea ikiwemo Tanzania hawafanyi hivyo kwa hisani bali wanatimiza wajibu wao,” amesema Kabudi. 

Amesema waliochafua mazingira lakini sasa wana mali za kutosha, wana wajibu wa kutoa fedha, teknolojia ya kupambana na  hali hiyo na nchi zilizobaki zina wajibu wa kushiriki katika miradi hiyo ili kunusuru na kuikoa dunia isiangamie mapema kuliko inavyotarajiwa.


Soma zaidi: Maoni: 


Aidha, amesema Tanzania inaungana na Katibu Mkuu wa UN, Antonio Guaterres katika kuhakikisha kwamba nchi zinazoendelea zinasaidiwa kupata maendeleo na wakati huo huo kuhifadhi mazingira. 

“Na maana yake wote tuna wajibu wa pamoja wa kulinda mazingira, lakini kila mtu ana wajibu ulio tofauti,” amesisitiza Kabudi. 

Tanzania imetenga asilimia 32 ya eneo la nchi kama hifadhi ya misitu ikiwa ni njia mojawapo ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV