TPDC yafungua fursa ya uwekezaji vituo vya gesi asilia Tanzania

July 19, 2019 2:29 pm · Daniel
Share
Tweet
Copy Link
  • Wajasiriamali wakaribishwa kujenga na kuuza gesi hiyo kwa watumiaji wa mwisho.
  • Vituo hivyo vitakuwa vinauza gesi kwa wamiliki wa magari yanayotumia rasilimali hiyo. 

Dar es Salaam. Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) limefungua milango kwa wajasiriamali  na kampuni kuwekeza katika ujenzi wa vituo vya kuuzia gesi asilia jijini Dar es Salaam kwa ajili ya magari yanayotumia nishati hiyo.

Wamiliki wa vituo hivyo watakuwa wananunua gesi hiyo kwa msambazaji mkuu na kuwafikishia watumiaji wa mwisho wakiwemo wamiliki wa magari yanayotumia gesi asilia. 

Kwa mujibu wa  tangazo lililotolewa TPDC kwa umma linaeleza kuwa  linatafuta mwekezaji atakayewekeza katika uchimbaji wa gesi na usambazaj gesi jijini humo kwa ajili ya magari.

“Kuanzia Julai Mosi TPDC itaanza kujenga mitambo mikubwa miwili katika jiji la  Dar es Salaam ambayo itasaidia usambazaji wa gesi (CNG) kwa vituo vidogo ambavyo vipo mbali na miundombinu ya bomba la mafuta,” inasomeka sehemu ya tangazo hilo.


Soma zaidi: Statoil yaja kivingine uchimbaji wa gesi Tanzania


Mwekezaji anatakiwa kuonyesha nia ya dhati na ushaidi wa uzoefu wake na uwezo wa kufanya hiyo kazi ya kusimamia vituo vya kuuza gesi ili aweze kupatiwa leseni na Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura) kwa mujibu wa sheria.

Licha ya kuonyesha nia, atawajibika kutoa taarifa zake za nyuma kuhusu kazi hiyo sambamba na muundo wa  wa uongozi katika kampuni yake.

Masharti mengine ni pamoja na kuwa na uwezo wa kifedha au utaratibu wa kutekeleza uwekezaji huo, kuhakikisha usalama wa umma ambapo mwekezaji anapaswa kuonyesha kuwa na ujuzi wa usalama wa afya na masuala ya mazingira kuhusiana na sekta ya mafuta. 

Pia utayari ya kutekeleza mpango wa maudhui ya ndani na masuala mengine ambapo atawajibika kusafirisha gesi hiyo kutoka mtambo mama hadi kituoni huku Ewura atabaki na jukumu la kupanga bei. 

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
21 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
21 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
21 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwanzo mwisho mapokezi ya Rais wa Namibia Netumbo Nandi Ikulu Dar es Salaam

Mwanzo mwisho mapokezi ya Rais wa Namibia Netumbo Nandi Ikulu Dar es Salaam

Nukta TV

Sikia kisa cha bibi wa Mbagala, chanzo Jaji Mkuu Masaju kupanda cheo

Sikia kisa cha bibi wa Mbagala, chanzo Jaji Mkuu Masaju kupanda cheo

Nukta TV

FAHAMU KUHUSU SIKOSELI | Part 1: Ugonjwa wa kurithi, unaotesa maelfu ya watoto Tanzania

FAHAMU KUHUSU SIKOSELI | Part 1: Ugonjwa wa kurithi, unaotesa maelfu ya watoto Tanzania

Nukta TV