Tanzania kuzalisha ajira milioni 6.5 sekta ya viwanda

June 30, 2025 5:34 pm · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Kati ya ajira hizo, milioni 1.04 ni za moja kwa moja.
  • Ajira hizo zitatoka kwenye viwanda 9,045 vitakavyojengwa.

Dar es Salaam. Waziri wa Viwanda na Biashara Dk Sulemani Jafo amesema Serikali inakusudia kujenda viwanda 9,045 vitavyozalisha ajira milioni 6.5, jambo litakalosaidia kuboresha maisha ya Watanzania na kuinua uchumi wa nchi.

Dk Jafo aliyekuwa akizungumza katika ufunguzi kaulimbiu mpya ya Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) mmoani Morogoro leo Juni 30, 2026 amesema kati ya ajira hizo zitakazozalishwa, milioni 1.04 ni za moja kwa moja ambazo zina mchango wa moja kwa moja na maisha ya Watanzania.

Aidha, Waziri amewataka maafisa biashara kusimamia mfumo wa stakabadhi ghalani ili kuwasaidia wakulima kupata bei stahiki za mazao yao.

Follow Us on TikTok

Subscribe to Our YouTube Channel

Subscribe

Loading videos...

Loading videos...

Loading videos...

Enable Notifications OK No thanks