Tanzania kuzalisha ajira milioni 6.5 sekta ya viwanda
June 30, 2025 5:34 pm ·
Mwandishi
- Kati ya ajira hizo, milioni 1.04 ni za moja kwa moja.
- Ajira hizo zitatoka kwenye viwanda 9,045 vitakavyojengwa.
Dar es Salaam. Waziri wa Viwanda na Biashara Dk Sulemani Jafo amesema Serikali inakusudia kujenda viwanda 9,045 vitavyozalisha ajira milioni 6.5, jambo litakalosaidia kuboresha maisha ya Watanzania na kuinua uchumi wa nchi.
Dk Jafo aliyekuwa akizungumza katika ufunguzi kaulimbiu mpya ya Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) mmoani Morogoro leo Juni 30, 2026 amesema kati ya ajira hizo zitakazozalishwa, milioni 1.04 ni za moja kwa moja ambazo zina mchango wa moja kwa moja na maisha ya Watanzania.
Aidha, Waziri amewataka maafisa biashara kusimamia mfumo wa stakabadhi ghalani ili kuwasaidia wakulima kupata bei stahiki za mazao yao.
Latest
12 hours ago
·
Lucy Samson
TMA: Mvua kubwa kunyesha kesho katika mikoa mitano
17 hours ago
·
Lucy Samson
Jenista Mhagama afariki dunia
2 days ago
·
Fatuma Hussein
Jeshi la Polisi: Hali ya usalama ni shwari Tanzania
2 days ago
·
Fatuma Hussein
Viwango vya kubadili fedha Tanzania Desemba 10, 2025