Soda au bia: Bidhaa gani huchangia zaidi kwenye mapato?
Dar es Salaam. Kila tukinunua sehemu kubwa ya bidhaa au huduma kuna asilimia 18 ya bei tunayolipa hukatwa kama Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) kwa mujibu wa sheria.
Hata hivyo, uliwahi kujiuliza ni bidhaa gani Tanzania Bara huchangia kwa kiwango kikubwa mapato katika kipengele hicho cha kodi?
Ripoti ya takwimu za kodi ya mwaka 2016/17Â iliyochapishwa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) inaonyesha bia ndiyo bidhaa inayochangia kwa kiwango kikubwa mapato ya VAT ikilinganishwa na bidhaa nyingine. Mapato ya kodi ni muhimu katika utoaji wa huduma za kijamii kama afya, elimu na ujenzi wa miradi ya maendeleo zikiwemo barabara.
Katika mwaka wa fedha wa 2016/17, bia zilichangia asilimia 30 ya mapato yote ya aina hiyo ya kodi. Hii ina maana kuwa Sh100 iliyokusanywa kwenye VAT, Sh30 ilichangiwa na bia.Â
Mchango huo wa bia kwenye mapato ya kodi ya VAT ni zaidi ya mara tatu na nusu ya yale yaliyokusanywa kutoka kwenye vinywaji baridi kama soda na juisi.
Fuatilia grafu hiyo kwa habari zaidi juu ya mchango wa bidhaa za ndani katika mapato nchini.
Â