Samaki wabichi, nyumba za kulala wageni vyachangia kupaisha mfumuko wa bei

July 8, 2019 2:30 pm · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • NBS yaeleza kuwa mfumuko wa bei kwa mwaka ulioishia Juni 2019 ulipaa hadi asilimia 3.7 kutoka 3.5 ya Mei mwaka huu.

Dar es Salaam. Kasi ya mabadiliko ya bei za bidhaa na huduma kwa mwaka ulioishia Juni mwaka huu imepaa hadi asilimia 3.7 kutoka asilimia 3.5 iliyorekodiwa Mei 2019 ikichagizwa zaidi na kuongezeka kwa bei za bidhaa za vyakula na zisizo za vyakula zikiwemo dagaa, samaki wabichi na mafuta.

Takwimu mpya za mfumuko wa bei zilizotolewa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) leo (9 Julai 8, 2019) zinabainisha kuwa baadhi ya bidhaa za vyakula zilizochangia kuongezeka kwa mfumuko wa bei ni pamoja na samaki wabichi kwa asilimia 27.3, unga wa mahindi (asilimia 3.6), unga wa ngano (asilimia 4.4), mtama (asilimia 4.9) na dagaa kwa asilimia 16.5.

Bidhaa hizo ni moja ya vyakula vikuu vinavyotumika zaidi nchini kwa familia za vipato vyote.

“Kwa upande mwingine baadhi ya bidhaa zisizo za vyakula zilizochangia kuongezeka kwa mfumuko wa bei wa Juni 2019 ni pamoja na dizeli kwa asilimia 11.4, petroli (asilimia 4.9), gharama za kulala kwenye nyumba za wageni (5.8) na vitabu vya shule kwa asilimia 2.4,” imeeleza taarifa ya NBS kwa vyombo vya habari.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.