Samaki wabichi, nyumba za kulala wageni vyachangia kupaisha mfumuko wa bei

July 8, 2019 2:30 pm · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • NBS yaeleza kuwa mfumuko wa bei kwa mwaka ulioishia Juni 2019 ulipaa hadi asilimia 3.7 kutoka 3.5 ya Mei mwaka huu.

Dar es Salaam. Kasi ya mabadiliko ya bei za bidhaa na huduma kwa mwaka ulioishia Juni mwaka huu imepaa hadi asilimia 3.7 kutoka asilimia 3.5 iliyorekodiwa Mei 2019 ikichagizwa zaidi na kuongezeka kwa bei za bidhaa za vyakula na zisizo za vyakula zikiwemo dagaa, samaki wabichi na mafuta.

Takwimu mpya za mfumuko wa bei zilizotolewa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) leo (9 Julai 8, 2019) zinabainisha kuwa baadhi ya bidhaa za vyakula zilizochangia kuongezeka kwa mfumuko wa bei ni pamoja na samaki wabichi kwa asilimia 27.3, unga wa mahindi (asilimia 3.6), unga wa ngano (asilimia 4.4), mtama (asilimia 4.9) na dagaa kwa asilimia 16.5.

Bidhaa hizo ni moja ya vyakula vikuu vinavyotumika zaidi nchini kwa familia za vipato vyote.

“Kwa upande mwingine baadhi ya bidhaa zisizo za vyakula zilizochangia kuongezeka kwa mfumuko wa bei wa Juni 2019 ni pamoja na dizeli kwa asilimia 11.4, petroli (asilimia 4.9), gharama za kulala kwenye nyumba za wageni (5.8) na vitabu vya shule kwa asilimia 2.4,” imeeleza taarifa ya NBS kwa vyombo vya habari.

Follow Us on TikTok

Subscribe to Our YouTube Channel

Subscribe

Loading videos...

Loading videos...

Loading videos...