Rais Kenyatta kuzuru Chato kwa mwaliko wa Magufuli

July 3, 2019 2:40 pm · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Atawasili Ijumaa Julai 5 katika uwanja wa ndege wa Chato mkoani Geita.
  • Atakutana na kufanya mazungumzo na Rais John Magufuli.

Dar es Salaam. Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta anatarajia kufanya ziara binafsi ya siku mbili nchini Tanzania itakayoanza Ijumaa, Julai 5 katika Wilaya ya Chato mkoani Geita ambako atakutana na kufanya mazungumzo na Rais John Magufuli ambaye yuko wilayani humo kwa ajili ya mapumziko. 

Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Gerson Msigwa leo (Julai 3, 2019) inaeleza kuwa Rais Kenyatta anakuja nchini kwa mwaliko wa Rais Magufuli.

Rais Kenyatta atatua katika uwanja wa ndege wa Chato saa 4:00 asubuhi na kisha kuelekea katika makazi ya Rais Magufuli yaliyopo katika kijiji cha Mlimani katika Wilaya hiyo iliyopo Kusini Magharibi mwa Tanzania. 

Akiwa nchini, Rais Kenyatta atafanya mazungumzo na mwenyeji wake kabla ya kurejea nchini Kenya. 

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.