Mwigulu alaani vitendo vvya uvunjifu wa amani

December 5, 2025 6:35 pm · Fatuma Hussein
Share
Tweet
Copy Link
  • Aonya wananchi dhidi ya wachochezi awataka kulinda amani ya Tanzania.

Dar es Salaam. Waziri Mkuu wa Tanzania, Dk Mwigulu Nchemba, amesema Serikali haitavumilia tena matukio ya uvunjifu wa amani kama yaliyojitokeza Oktoba 29, 2025, akisisitiza kuwa Tanzania itaendelea kuwa nchi ya utulivu na mshikamano.

Dk Mwigulu aliyekuwa akizungumza leo Disemba 5, 2025, mara baada ya kukagua ofisi ya Mtendaji wa Kata ya Kisesa jijini Mwanza  iliyochomwa moto Oktoba 29, 2025 amesema Serikali imejipanga kuchukua hatua kali dhidi ya wanaochochea vitendo vya uvunjifu wa amani.

“Tuna nchi nzuri inaitwa Tanzania, tuilinde. Tusimpe adui mwanya kupitia mavuguvugu haya….; sisi hatutaruhusu vuguvugu wala vurugu. Anayetaka fujo asimtangulize mtoto wa mtu, aende yeye mwenyewe,” alisema Mwigulu.

Aidha, Mwigulu ameonya vijana kufuata mkumbo akiwataka kutokubali kutumiwa kuchoma mali za wananchi au kusababisha uharibifu huku wahusika wakuu wakibaki mafichoni.

Kwa upande wake, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro, amewataka Watanzania kutoshabikia vurugu kwa kuwa zina gharama kubwa kiusalama na kiuchumi.

Muliro amesema Jeshi la Polisi linafahamu kuwa linawatumikia wananchi na jukumu lake ni kulinda amani hivyo amewataka wananchi kuzingatia sheria.

Ikumbukwe kuwa katika uchaguzi uliofanyika oktoba 29, 2025, nchini Tanzania kulitokea maandamano yaliopelekea uvunjifu wa amani na kusababisha maafa kwa watu ikiwemo kupoteza mali na maisha.

Hata hivyo, Novemba 18, 2025, Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan aliunda tume ya watu saba kuchunguza matukio ya uvunjifu wa amani yaliyotokea nchini wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu.

Pia, katika mkutano wake na wazee wa Dar es Salaam Desemba 2, 2025, alieleza kuwa matukio ya Oktoba 29 yalikuwa mradi mkubwa wenye nia ovu uliokuwa na wafadhili, washirika na watekelezaji waliodhamiria kuhujumu Serikali huku wengine wakifuata mkumbo.

Rais Samia alisisitiza kuwa kilichotokea si maandamano bali ni vurugu, kwa sababu maandamano ya kisheria ni lazima yawe na kibali, kueleza njia yatakayopita, na kulindwa na Polisi.

Naye, mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, amewataka wananchi kuiamini tume hiyo na kuipa muda kufanya kazi yake.

/
No matches found for this filter
22 May, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
23 May, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
23 May, 2026
No active movers today
Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
MIKOA YA KIPOLISI ILIYOONGOZA KWA MATUKIO BARABARANI TANZANIA BARA 2025

MIKOA YA KIPOLISI ILIYOONGOZA KWA MATUKIO BARABARANI TANZANIA BARA 2025

Nukta TV

🔴LIVE: KAPINGA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA 2026/2027 BUNGENI.

🔴LIVE: KAPINGA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA 2026/2027 BUNGENI.

Nukta TV

MIKOA 5 ILIYOONGOZA KWA MATUKIO BARABARANI 2025 TANZANIA BARA

MIKOA 5 ILIYOONGOZA KWA MATUKIO BARABARANI 2025 TANZANIA BARA

Nukta TV