Mwaka ambao simu za mkononi zilizipiga bao simu za mezani
- Mwaka 1995 ilikuwa ni anasa kumiliki simu ya mkononi.
- Wakati huo, watumiaji wa simu za mkononi walikuwa 2,198 kati ya watumiaji 90,298 waliokuwepo nchini.
Dar es Salaam. Mwaka 1995 ilikuwa ni anasa kumiliki simu ya mkononi. Kati ya watumiaji 100 wa simu, ni takriban watatu tu walikuwa wakitumia simu za mkononi kwa mujibu wa takwimu za Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA).
Wakati huo, watumiaji wa simu za mkononi walikuwa 2,198 kati ya watumiaji 90,298 waliokuwepo nchini. Enzi hizo huduma za simu za mezani ilikuwa kila kitu kutokana na simu za mkononi kuwa ghali na teknolojia kutofika katika maeneo mengi Tanzania.
Simu za mkononi zimechangia kwa kiasi kubwa kuleta maendeleo nchini kwa kuongeza kasi ya mawasiliano huku mapinduzi makubwa yakitokea baada ya kuanza kutoa huduma za kifedha.

Latest