Mkombozi Bank yapata bosi mpya

January 24, 2018 6:43 am · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link

  • Ni kigogo aliyewahi kufanya kazi katika benki za NMB, Exim na Standard Chartered.
  • Anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Edwina Lupembe aliyestaafu.

Dar es Salaam. Sekta ya benki nchini imempokea bosi mpya, baada ya Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya biashara ya Mkombozi kumteua George Shumbusho kuwa Mkurugenzi Mtendaji mpya kuanzia kuanzia Desemba mosi, 2017.  

Shumbusho, ambaye ni moja ya watu maarufu katika sekta hiyo ya fedha, anachukua nafasi ya iliyoachwa wazi na Edwina Lupembe aliyestaafu Desemba 31 mwaka jana baada ya kuhudumu benki hiyo tangu Agosti 2009.

Edwina alikuwa moja ya vigogo wachache wanawake katika sekta ya benki nchini akiwa sambamba na wenzie kama Ineke Bussemeker wa NMB, Jacqueline Woiso wa Bank M na Mwanahiba Mzee wa Eco Bank.

Taarifa kwa umma iliyotolewa na Menejimenti ya Bodi katika vyombo vya habari leo, Januari 24, 2017 imemshukuru Lupembe kwa kazi yake nzuri ya mfano aliyoifanya katika miaka minane aliyoongoza benki hiyo iliyooanzishwa na Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC) mwaka 2009.

“Bodi ina imani kuwa mkurugenzi mpya atatumia uzoefu wake wa kitaaluma kwa kufanya kazi karibu na wafanyakazi wa benki, Bodi na wadau wengine katika kuindeleza benki yetu wakati wa uongozi wake,” inasomeka sehemu ya taarifa hiyo.

Kabla ya uteuzi huo mpya katika benki hiyo inayotoa huduma za mikopo kwa wafanyabiashara wadogo, wa kati na wakubwa, Shumbusho alishawahi zitumikia benki kubwa nchini zikiwemo Exim Bank, Stanbic Bank, Standard Chartered na NMB.

Shumbusho mwenye shahada ya uzamili ya biashara (MBA) kutoka Shule ya Usimamizi wa Biashara ya Maastricht nchini Uholanzi, ni mtaalamu wa masoko na huduma za kibenki.

Kigogo huyo anaingia kuiongoza benki hiyo katika kipindi ambacho sekta ya benki inakabiliwa na changamoto lukuki ikiwemo kuongezeka kwa mikopo chechefu kutoka asilimia 9.1 Septemba 2016 hadi asilimia 12.5 Septemba, 2017, kwa mujibu wa Wizara ya Fedha na Mipango. Mwenendo huo umekuwa ukitishia mustakabali wa benki nyingi nchini hususan zenye mitaji midogo.

Mkombozi Bank ni moja ya benki muhimu kwa ukuzaji wa biashara nchini kutokana na kutoa huduma za mikopo ya vikundi, kilimo, biashara, vifaa na uwekezaji na mikopo inayotokana na dhamana ya mishahara.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.