Maumivu yaja kwa wacheza michezo ya kubahatisha

June 14, 2019 12:39 pm · Daniel
Share
Tweet
Copy Link
  • Serikali imebuni mfumo wa kudhibiti michezo hiyo ili kujipatia zaidi mapato ya kodi.
  • Pia utadhibiti udangajifu unaofanywa na waendeshaji wa michezo hiyo. 

Dar es Salaam. Serikali imebuni na kutengeneza mfumo wa kudhibiti michezo ya kubahatisha maarufu kama ‘betting’ ikiwa ni hatua ya kuongeza mapato baada ya kuonekana una muitikio mkubwa wa watu hasa vijana. 

Hatua hiyo inakuja ikiwa imepita miezi sita tangu Makamu Mwenyekiti wa dhehebu la Mabohora, Zainuddin Adamjee kulalamika mbele ya Rais John Magufuli, Ikulu jijini Dar es Salaam kuwa nguvukazi ya Taifa inapotea kwa sababu vijana wengi hawafanyi kazi na wanatumia muda mwingi kucheza michezo hiyo kwenye mitandao ya kijamii. 

Wakati akiwasilisha mapendekezo ya bajeti ya Serikali kwa mwaka 2019/2020, Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango amesema kuwa kutokana wimbi la vijana wengi kujihusisha na michezo ya kubahatisha na kusahau majukumu ya ujenzi wa Taifa,  Serikali imependekeza kutengeneza mfumo maalum wa kudhibiti uendeshaji wa michezo hiyo. 

“Serikali ikishirikiana na Bodi ya Michezo ya Kubahatisha imebuni na kutengeneza mfumo maalum ambao utatumika kudhibiti uchezaji  wa michezo hii (Responsible Gaming),’ amesema Dk Mpango.

Waziri huyo amesema Serikali imependekeza mfumo huu kutumika ili kudhibiti udanganyifu ambao unafanywa na waendeshaji wa michezo ya kubahatisha na kuikosesha Serikali mapato.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
17 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
17 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Siku ya Familia, Mtoto wa Afrika kuadhimishwa Juni 30, 2026

Siku ya Familia, Mtoto wa Afrika kuadhimishwa Juni 30, 2026

Nukta TV

Wadau wa 'kubet" watoa ya moyoni, pendekezo kupanda kwa tozo 5%

Wadau wa 'kubet" watoa ya moyoni, pendekezo kupanda kwa tozo 5%

Nukta TV

Wasemayo wananchi, vocha za kukwangua kupigwa maruku mijini

Wasemayo wananchi, vocha za kukwangua kupigwa maruku mijini

Nukta TV