Kicheko kwa wafanyabiashara wanaopata TIN kwa mara ya kwanza

June 14, 2019 9:48 am · Daniel
Share
Tweet
Copy Link
  • Serikali inapendekeza kutoa unafuu wa kutolipa kodi kwa kipindi cha miezi sita kuanzia wakati mfanyabiashara au mwekezaji anapopewa Namba ya Utambulisho wa Mlipakodi (TIN).
  • Itaondoa usumbufu au dhana ya woga wakati wa kuanzisha biashara.

Dar es Salaam. Kama unakusudia kuanzisha biashara katika siku za hivi karibuni na umekuwa ukihofia kuanza kukatwa kodi wakati biashara yako ikiwa changa, sasa una kila sababu ya kutabasamu, baada ya Serikali kutoa ahueni ya kodi. 

Serikali imetangaza kusudio la kutoa nafuu ya kutolipa kodi kwa kipindi cha miezi sita kuanzia wakati mfanyabiashara au mwekezaji anapopewa Namba ya Utambulisho wa Mlipakodi (TIN). 

Akizungumza jana bungeni wakati akiwasilisha bajeti ya Serikali Kuu kwa mwaka 2019/2020,  Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango amesema hatua hii inatofautiana na hali ilivyo sasa ambapo mfanyabiashara anapopewa TIN anaanza kufanyiwa tathmini (tax assessment) ya mapato yake ya biashara na kutakiwa kulipa kodi. 

“Hatua hii itawezesha wafanyabiashara na wawekezaji wapya kupata muda wa kujiandaa na mahitaji yanayotakiwa katika shughuli wanazofanya na kuondoa usumbufu au dhana ya woga wakati wa kuanzisha biashara,” amesema Waziri Mpango. 

Amesema katika kipindi hicho mfanyabiashara anakuwa anashughulikia  mahitaji ya Leseni ya biashara na vibali vingine muhimu vya biashara, jambo litakamsaidia kujipanga kabla hajaanza kulipa kodi.

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.