Kicheko kwa wafanyabiashara wanaopata TIN kwa mara ya kwanza

June 14, 2019 9:48 am · Daniel
Share
Tweet
Copy Link
  • Serikali inapendekeza kutoa unafuu wa kutolipa kodi kwa kipindi cha miezi sita kuanzia wakati mfanyabiashara au mwekezaji anapopewa Namba ya Utambulisho wa Mlipakodi (TIN).
  • Itaondoa usumbufu au dhana ya woga wakati wa kuanzisha biashara.

Dar es Salaam. Kama unakusudia kuanzisha biashara katika siku za hivi karibuni na umekuwa ukihofia kuanza kukatwa kodi wakati biashara yako ikiwa changa, sasa una kila sababu ya kutabasamu, baada ya Serikali kutoa ahueni ya kodi. 

Serikali imetangaza kusudio la kutoa nafuu ya kutolipa kodi kwa kipindi cha miezi sita kuanzia wakati mfanyabiashara au mwekezaji anapopewa Namba ya Utambulisho wa Mlipakodi (TIN). 

Akizungumza jana bungeni wakati akiwasilisha bajeti ya Serikali Kuu kwa mwaka 2019/2020,  Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango amesema hatua hii inatofautiana na hali ilivyo sasa ambapo mfanyabiashara anapopewa TIN anaanza kufanyiwa tathmini (tax assessment) ya mapato yake ya biashara na kutakiwa kulipa kodi. 

“Hatua hii itawezesha wafanyabiashara na wawekezaji wapya kupata muda wa kujiandaa na mahitaji yanayotakiwa katika shughuli wanazofanya na kuondoa usumbufu au dhana ya woga wakati wa kuanzisha biashara,” amesema Waziri Mpango. 

Amesema katika kipindi hicho mfanyabiashara anakuwa anashughulikia  mahitaji ya Leseni ya biashara na vibali vingine muhimu vya biashara, jambo litakamsaidia kujipanga kabla hajaanza kulipa kodi.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
14 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV