Faida, jinsi ya kuandaa juisi ya papai na ndizi

October 30, 2024 4:13 pm · Mlelwa Kiwale
Share
Tweet
Copy Link
  • Kwa wale wanaosumbuliwa na matatizo ya choo kigumu, wagonjwa au watoto wanaoanza kujifunza kula juisi hii ndio yenyewe.

Inawezekana umeshawahi kunywa aina nyingi za juisi zilizoburudisha koo lako na kukupa virutubisho vilivyojenga na kuimarisha afya ya mwili wako.

Sasa katika orodha yako ya aina ya juisi ulizowahi kunywa ongeza na juisi ya papai na ndizi itakayokuburudisha huku ikikupa faida lukuki za kiafya.

Kwa wale wanaosumbuliwa na matatizo ya choo kigumu, wagonjwa au watoto wanaoanza kujifunza kula hii ndio yenyewe.

Maandalizi

Osha papai na ndizi kwa maji safi kisha uanze kumenya na kukatakata kwa saizi ndogo itakayoweza kusagika kwa haraka.

Ukimaliza andaa blenda na uweke mahitaji yako yote pamoja na vipande vya barafu kama unapendelea kisha usage mpaka matunda yote yachanganyike vizuri.

Kama juisi ni nzito sana unaweza kuongeza maji kidogo kidogo au maziwa mpaka upate uzito unaopendelea kisha juisi yako itakuwa tayari kwa kunywa.

Unaweza pia kuichuja lakini kama umeisaga kwa muda mrefu papai na ndizi huwa zinasagika vizuri na hazina nyuzi nyuzi.

Ikiwa hupendelei sukari unaweza usiweke na bado juisi yako ikawa tamu.

/
No matches found for this filter
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
5 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
5 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Unaweza kusema ni maumivu juu ya maumivu kwa watumiaji wa vyombo vya moto vinavyotumia mafuta ya

Nukta TV

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Neema Mohamed, Mkurugenzi wa Bone and Blood Foundation, ni shujaa wa ugonjwa wa selimundu Sickl

Nukta TV

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ametua kwenye ardhi ya Urusi kwa ziara ya kitaifa ya siku

Nukta TV