Facebook yabuni mfumo mpya wa kupambana na matapeli mtandaoni

July 19, 2019 12:18 pm · Daniel
Share
Tweet
Copy Link
  • Amebuniwa baada ya kushtakiwa na mwanzilishi wa Money Saving Expert, Martin Lewis.
  • Unasaidia kubaini na kudhibiti matangazo yasiyo halisi.
  • Unasaidia kuwaepusha watu na wizi mtandaoni unaofanywa na matapeli.

Wiki hii mtandao wa kijamii wa facebook umeanzisha mfumo mpya wa kubaini na kudhibiti matangazo bandia  yanayotumia na baadhi ya watu kufanya utapeli mtandaoni.

Mfumo huo mpya unakuja baada ya mtandao huo kushtakiwa  Aprili, 2018 na mwazilishii wa tovuti ya matangazo ya  Money Saving Expert, Martin Lewis kuhusu picha zake kutumiwa kwenye matangazo bandia yaliyowekwa kwenye mtandao huo wa kijamii.

Martin amesema matangazo hayo yaliharibu heshima yake kwenye jamii lakini mwanzoni mwa mwaka huu aliamua kuachana na kesi hiyo dhidi ya Facebbok kwa masharti mawili.


Zinazohusiana:Facebook kuanza kuwachaguliwa wafuasi wake viongozi wa makundi


Aliitaka Facebook ichangie Paundi milioni 3 sawa na takriban Sh8.6 bilioni kwa ajili ya kuanzisha programu ya kupambana na udanganyifu nchini Uingereza na uazishwaji wa laini ya simu (Citizen Advice Scam Action (CASA)) kwa ajili ya kuwasaidia watu wanapokutana na udanganyifu au utapeli mtandaoni.

Ili kuweza kutumia programu hiyo, utalazimika kwenda upande wa kulia wa mtandao huo wa facebook kwenye kila tangazo ambapo utakutana na alama za nukta itatu  ukiponyeza utapata  maelezo ya kuripoti tangazo bandia (Misleading or Scam) ambayo yatasaidia Facebook kupitia malalamiko yako na kuyafanyia kazi. 

Huenda mfumo huo ukawasaidia watu wengi ambao wamekuwa wakikutana na matapeli au watu wenye nia mbaya ya kujipatia fedha kwa njia isiyo halali kwa kutumia mtandao wa Facebook. 

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

🔴LIVE: RAIS SAMIA ANAZINDUA MELI YA KWANZA YA UVUVI WA BAHARI KUU

Nukta TV

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Kwa nini wanawake wako katika hatari zaidi kupata magonjwa ya akili?

Nukta TV

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

🔴LIVE: HOMERA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA BUNGENI

Nukta TV

BENEFIT FROM
Nukta ADS
Advertise with us to reach a wider audience with high conversion rates.
Other Nukta Africa Products
Nukta Habari
Stories that matter
Topics
Inuldge yourself with the topics in Nukta
All
Business
Africa
Contact
Tel
+255 750 881 888
Mail
newsroom@nukta.co.tz
Address
Mwananyamala kwa Kopa Dabe House Dar es Salaam TZ, 14108
Social Media

© 2024 Nukta Africa. All Rights Reserved.