Daladala ni kila kitu usafiri Tanzania

January 23, 2019 6:04 pm · Daniel Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni asilimia 85.7 ya mabasi yote yaliyopo nchini na hutumika zaidi kusafirisha abiria katika miji na vijiji.
  • Kwa kila daladala tano zilizopo Tanzania, moja ipo mkoa wa Dar es Salaam.

Dar es Salaam. Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Kamwelwe amesema Tanzania ina mabasi 49,000 ambapo kati ya hayo 7,000 ni mabasi yanayofanya safari zake mikoani na yanayobaki ambayo ni sawa na asilimia 85.7 ni daladala zinazofanya safari zake ndani ya miji. 

Katika hotuba yake ya Desemba 20, 2018 wakati wa uzinduzi wa ujenzi wa daraja la kisasa la Salender litakalopita juu ya Bahari  ya Hindi na kupunguza adha ya foleni jijini Dar es salaam, alisema katika daladala zote zilizopo nchini, 9,000 zinapatikana mkoa wa Dar es Salaam, ambapo zikiwekewa mikakati mizuri zinaweza kuwa sehemu ya kukuza mapato ya Serikali. 

Kwa takwimu hizo, inamaanisha kuwa kwa kila daladala tano zilizopo Tanzania, moja ipo mkoa wa Dar es Salaam.

Kamwelwe alisema hadi mwishoni mwa Januari 2019 mabasi yote yanatakiwa kutumia mfumo wa utoaji wa tiketi za kielektroniki kwa abiria ili kurahisisha upatikanaji wa kodi ya Serikali.

Mwaka 2017 sekta ya uchukuzi ilikuwa ni moja zilizofanya vyema baada ya kuchangia asilimia 16.5 ya Pato la Taifa (GDP) ikiwa nyuma kidogo ya sekta ya utalii ambayo ilichangia asilimia 17.2.

 

Follow Us on TikTok

FOLLOW NOW

Subscribe to Our YouTube Channel

SUBSCRIBE NOW