Dola yapungua nguvu dhidi ya Shilingi ya Tanzania
- Mabadiliko ya leo yanaonesha mwelekeo wa kushuka kwa baadhi ya sarafu za kigeni, huku Dola ikiwa na mabadiliko madogo zaidi ukilinganisha na Rand na Euro.
Dar es Salaam. Dola ya Marekani imeanza Septemba kwa kupunguza nguvu dhidi ya Shilingi ya Tanzania, baada ya bei yake ya kununuliwa katika Benki ya NMB kushuka kwa asilimia 0.38 ukilinganisha na viwango vilivyotumika Agosti 30, 2026.
Kwa upande wa Dola ya Marekani leo Septemba 2, 2026, NMB imenunua kwa Sh 2,590 kutoka Sh2,600 iliyokuwa ikitumika mwishoni mwa wiki iliyopita ikiwa imepungua kwa asilima 0.38 huku bei ya kuuza ikishuka kutoka Sh2,680 hadi Sh2,670.
Kwa upande wa Benki ya CRDB, imeendela kutumia viwango vile vile vilivyokuwa vikitumika Agosti 31, 2026 vya kununua kwa Sh2,605 na kuuza kwa Sh2,685.
Sarafu nyingine kama Rand ya Afrika Kusini (ZAR) kwa CRDB inanunuliwa kwa Sh153.96 kutoka Sh155.34 ikiwa imeshuka kwa asilimia 0.89, huku NMB ikishusha kutoka Sh163 hadi Sh161, sawa na asilimia 1.23.
Kwa ujumla, mabadiliko ya leo yanaonesha mwelekeo wa kushuka kwa baadhi ya sarafu za kigeni, huku Dola ikiwa na mabadiliko madogo zaidi ukilinganisha na Rand na Euro.
