Polisi Tanzania yamnasa mwanajeshi wa Marekani akiwa na mabomu manne 

November 17, 2025 11:36 am · Kelvin Makwinya
Share
Tweet
Copy Link
  • Polisi yasema inaendelea kukusanya ushahidi na kumhoji mtuhumiwa.

Dar es Salaam. Jeshi la Polisi nchini limesema limemkamata Charles Onkuri Ongeta, mwenye uraia pacha wa Marekani na Kenya na cheo cha Sajenti katika Jeshi la Marekani, akidaiwa kuingia nchini akiwa na mabomu manne ya kurushwa kwa mkono aina ya CS M68.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Polisi wa mkoa huo, Mark Njera tukio hilo limetokea Novemba 16, 2025 majira ya saa 6:00 mchana katika eneo la mpaka la Sirari, wakati mtuhumiwa akijaribu kuingia Tanzania akitokea Kenya kwa kutumia gari aina ya Toyota Landcruiser.

Kwa mujibu wa Njera, silaha hizo ni marufuku kuingizwa nchini kwa mujibu wa sheria za Tanzania.

“Kwa mujibu wa sheria ya umiliki wa silaha, mabomu ya aina hii hayaruhusiwi kabisa kuingizwa nchini. Hata kama angeomba kibali, asingeruhusiwa kuyapitisha,” amefafanua

Jeshi la Polisi limesema, linaendelea kukusanya ushahidi na kumhoji mtuhumiwa kuhusu tuhuma hizo, kabla ya kuchukua hatua stahiki kwa mujibu wa sheria.

/
No matches found for this filter
22 May, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
23 May, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
23 May, 2026
No active movers today
Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
MIKOA YA KIPOLISI ILIYOONGOZA KWA MATUKIO BARABARANI TANZANIA BARA 2025

MIKOA YA KIPOLISI ILIYOONGOZA KWA MATUKIO BARABARANI TANZANIA BARA 2025

Nukta TV

🔴LIVE: KAPINGA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA 2026/2027 BUNGENI.

🔴LIVE: KAPINGA AKIWASILISHA HOTUBA YA BAJETI YA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA 2026/2027 BUNGENI.

Nukta TV

MIKOA 5 ILIYOONGOZA KWA MATUKIO BARABARANI 2025 TANZANIA BARA

MIKOA 5 ILIYOONGOZA KWA MATUKIO BARABARANI 2025 TANZANIA BARA

Nukta TV