Mawaziri Wakuu wa Tanzania tangu uhuru

Dar es Salaam. Tangu Tanganyika ilipopata uhuru mwaka 1961, nafasi ya Waziri Mkuu imekuwa mhimili muhimu katika uendeshaji wa serikali na utekelezaji wa sera za taifa. Kuanzia kwa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Waziri Mkuu wa kwanza wa Tanganyika, hadi kwa Kassim Majaliwa Majaliwa, Waziri Mkuu wa sasa.
Tanzania imepitia viongozi waliotoa mchango mkubwa katika kuimarisha utawala, uchumi, na amani ya nchi. Wengine waliowahi kushika nafasi hiyo ni pamoja na Rashidi Kawawa, Edward Sokoine, Cleopa Msuya, Salim Ahmed Salim, Joseph Warioba, John Malecela, Frederick Sumaye, Edward Lowassa, na Mizengo Pinda.
Kila mmoja ameacha alama katika historia ya uongozi wa taifa, lakini je, ni nani atakwenda kurithi nafasi hiyo kutoka kwa Waziri Mkuu wa sasa Kassim Majaliwa ?
Latest