SAU na ndoto ya kumaliza tatizo la ajira nchini

September 9, 2025 8:08 pm · Lucy Samson
Share
Tweet
Copy Link
  • Yasema itamaliza tatizo hilo kupitia sekta ya kilimo, viwanda na teknolojia.

Arusha. Chama cha Sauti ya Umma (SAU),  kimezindua kampeni zake kwa nafasi ya urasi, ubunge na udiwani huku kikiahidi kupambana na tatizo la ukosefu wa ajira nchini ikiwa kitapewa ridhaa ya kuongoza nchi kwa miaka mitano ijayo.

Mgombea Urais wa wa Tanzania kupitia Chama cha SAU, Majalio Kyara aliyekuwa akizungumza na katika uzinduzi wa kampeni hizo Ukonga, Dar es Salaam leo Septemba 9, 2025 amesema chama hicho kitatengeneza mfumo utakaotambua vipaji vya vijana ili kupambana ukosefu wa ajira.

“Vijana wengi wanakosa ajira kwasababu hakuna mfumo sahihi wa kuwezakutambua vipaji vya vijana wetu sisi kama SAU tunataka kutengeneza mfumo madhubuti ukaoweza kutambua vipaji vya vijana wetu…

… Mfumo huo utambue vipaji uvilee, uvikuze ili viweze kusaidia katika mandeleo ya mtu mmoja mmoja ya Taifa letu.

Mgombea huyo ametoa ahadi hiyo wakati ambapo idadi ya  wahitimu wa shule na vyuo inaongezeka kila mwaka huku nchini Tanzania huku nafasi za ajira zikiwa chache jambo linaloongeza idadi ya vijana wasio na ajira Tanzania.

Mgombea Urais wa wa Tanzania kupitia Chama cha SAU, Majalio Kyara akiwasili katika uzinduzi wa kampeni za chama hicho.Picha?TBC online

Kyara amebainisha kuwa chama hicho kina vipaumbele vitatu ambavyo ni kilimo, viwanda na teknolojia ambavyo vyote vikitumiwa vyema vinaweza kumaliza kabisa tatizo hilo la ajira.

“Kupitia kilimo tunakwenda kutatua changamoto nyingi kwenye Taifa letu ikiwemo afya, ajira na mambo mengine mengi hata uchumi wa Taifa na uchumi wa mwananchi mmoja mmoja.

Kwa upande wake mgombea mweza wa nafasi ya urais kupitia chama hicho Satia Bebwa amewataka wananchi waliohudhuria kampeni hizo kupiga kura za ndio kwa chama hicho kwa wingi ili waweze kutekeleza ahadi mbalimbali ikiwemo kutoa elimu bure, uzazi bure kwa wajawazito na pembejeo kwa wakulima.

“Hatutaki mzaha kwa sasa hivi tunataka kufanya kazi ajili yenu. Tupeni kura muone tutakachokifanya, hatutakaa mjini tutakaa pembezoni mwa mji ili tujue matatizo yenu,” amesema Bebwa

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV