Gumzo Bungeni: Magari ya Serikali kuwepo maeneo ya starehe

April 8, 2024 12:49 pm · admin
Share
Tweet
Copy Link
  • Ni magari yanayopaki maeneo hayo baada ya muda wa kazi. 
  • Wabunge wahoji ni lini tabia hiyo itakoma.
  • Serikali yasema itachukua hatua. 

Dar es salaam. Serikali imetoa onyo kwa watumishi wa umma kutumia magari yake kwa matumizi binafsi ikiwemo kupaki sehemu za starehe mara baada ya saa za kazi kwani ni kinyume na sheria.

Naibu Waziri wa Ujenzi Godfrey Kasekenya aliyekuwa akizungumza leo Aprili 8, 2024 Bungeni jijini Dodoma amesema, Serikali kupitia Waraka wa Rais Na.1 wa mwaka 1998 wa kubana matumizi ilielekeza kuwa magari yote ya Serikali yanatakiwa kuwa yameegeshwa sehemu zilizotengwa ifikapo saa 12:00 jioni. 

Ameongeza kuwa kama siyo muda wa kazi  inatakiwa magari hayo yawe na kibali rasmi kinachoruhusu kuwepo barabarani baada ya saa 12:00 jioni.

“Serikali kupitia Kanuni namba 21 Kanuni za Kudumu za Utumishi wa Umma za mwaka 2009, imezuia watumishi wa umma kutumia magari ya Serikali kwa matumizi binafsi…

“… mtumishi anayekwenda kinyume na maelekezo hayo anatakiwa kuchukuliwa hatua kali za kinidhamu,” amesema Kasekenya.

Naibu Waziri huyo ametoa ufafanuzi huo wakati akijibu swali la Mbunge wa Arumeru Magharibi Noah Saputu aliyetaka kujua ni lini Serikali itazuia kupaki magari ya Serikali sehemu za starehe baada ya saa za kazi.

Naye Mbunge wa Makete, Festo Sanga akiuliza swali la nyongeza amesema kanuni zipo lakini bado tabia hiyo haijakoma kwa baadhi ya watumishi. 

“Licha ya kwamba sheria na kanuni zimekuwepo zikizuia kama ambavyo mheshimiwa Naibu Waziri amesema lakini bado kwenye mitaa, kwenye baa na maeneo mengine magari ya Serikali yamekuwa yakionekana majira ya usiku.

“Upi mkakati wa Serikali kuhakikisha inazuia kabisa uwepo wa magari maeneo hayo kwa sababu imekuwa ni kero kwa wananchi lakini pia inaonesha ni matumizi mabaya ya fedha za Serikali?,” amehoji  Sanga.

Akijibu swali hilo, Kasekenya amesema kwa kuwa sheria, kanuni na taratibu zipo, wahusika wanatakiwa kusimamia ipaswavyo sheria hizo ili kudhibiti suala hilo.

“Tunawakumbusha na kuwasisitiza maafisa masuuli na waajiri wote wanaohusika waweze kuchukua hatua,” amesema Kasekenya.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV