Ziara ya Rais Magufuli Ruvuma yamng’oa kigogo wa halmashauri

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma, Dk Oscar Mbyuzi aliyefutwa kazi na Rais Magufuli leo. Picha|Mtandao.
- Ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma, Dk Oscar Mbyuzi ambaye uteuzi wake umetenguliwa leo na nafasi yake imechukuliwa na Jimson Mhagama.
- Sababu za kutenguliwa kwa Mmkurugenzi huyo bado hazijatajwa.
Dar es Salaam. Rais John Magufuli leo ametengua uteuzi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma, Dk Oscar Mbyuzi.
Taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu leo (Aprili 9, 2019) inaeleza kuwa kufuatia uamuzi huo, Rais Magufuli amemteua Jimson Mhagama kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo ambapo uteuzi wa Mhagama unaanza mara moja.
Hata hivyo, taarifa hiyo haijaweka bayana sababu za kigogo huyo kutolewa katika nafasi hiyo.
Mabadiliko hayo ya uongozi yanakuja wakati Rais Magufuli akikamilisha ziara ya siku sita mkoani Ruvuma aliyoanza tangu Aprili 4 mwaka huu ambapo leo anazindua kituo cha afya cha Madaba kilichopo Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.
Akiwa mkoani humo, Rais ametumia muda wake mwingi kuwaonya viongozi wa Serikali wakiwemo wakuu wa wilaya kutimiza majukumu yao kikamilifu na kuhakikisha wanawatumikia wananchi kwa kuwaondolea shida zao ikiwemo kuboresha huduma za kijamii. Â
Latest