Rais Kenyatta kuzuru Chato kwa mwaliko wa Magufuli

July 3, 2019 2:40 pm · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link
  • Atawasili Ijumaa Julai 5 katika uwanja wa ndege wa Chato mkoani Geita.
  • Atakutana na kufanya mazungumzo na Rais John Magufuli.

Dar es Salaam. Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta anatarajia kufanya ziara binafsi ya siku mbili nchini Tanzania itakayoanza Ijumaa, Julai 5 katika Wilaya ya Chato mkoani Geita ambako atakutana na kufanya mazungumzo na Rais John Magufuli ambaye yuko wilayani humo kwa ajili ya mapumziko. 

Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Gerson Msigwa leo (Julai 3, 2019) inaeleza kuwa Rais Kenyatta anakuja nchini kwa mwaliko wa Rais Magufuli.

Rais Kenyatta atatua katika uwanja wa ndege wa Chato saa 4:00 asubuhi na kisha kuelekea katika makazi ya Rais Magufuli yaliyopo katika kijiji cha Mlimani katika Wilaya hiyo iliyopo Kusini Magharibi mwa Tanzania. 

Akiwa nchini, Rais Kenyatta atafanya mazungumzo na mwenyeji wake kabla ya kurejea nchini Kenya. 

Enable Notifications OK No thanks