Facebook waja na hiki kwa watumiaji wenye wafuasi wengi

July 6, 2019 1:44 pm · Mwandishi
Share
Tweet
Copy Link

Dar es Salaam. Mtandao wa kijamii wa Facebook umeanzisha kipengele cha kuwatumia ujumbe marafiki wa karibu (Top pages) ili kumwezesha mtumiaji wake kuwasiliana kwa ukaribu na marafiki zake.

Kipengele hicho kinaweza kuwa ni moja ya huduma za kuvutia kwa watumiaji wa mtandao huo ulimwenguni ambao kwa sasa unakadiriwa kuwa na watumiaji bilioni 2. 

Hata hivyo, siyo kila mtumiaji wa Facebook atanufaika na huduma hiyo.

Watumiaji wa Facebook watakaonufaika na kipengele hicho ni wale ambao wana wafuasi kuanzia 10,000 (10k followers) huku sifa nyingine ukihitajika kuwa na umri kuanzia miaka 28.

Kupitia kipengele hicho mtumiaji wa Facebook ataweza kuwashukuru  mashabiki wake maarufu au kuwatumia habari za kipekee ambazo wafuasi wake wengine hawataweza kuzipata.

Mabadiliko hayo tayari yameanza kuonekana kwa baadhi ya watumiaji wa mtandao huo ulimwenguni kuanzia mwezi uliopita huku ikitarajiwa kuwafikia watu wengine wakati wowote.

Kipengele hicho kinachohusisha mashabiki  wa karibu (Top Fans) kinaweza kuwa ni fursa nyingine kwa mtumiaji wa Facebook kuweza kujenga mahusiano bora na marifiki zao wa karibu katika jamii wanazoishi.

Hii ni moja ya huduma za hivi karibuni katika uboreshaji wa mtandao huo ambao unakabiriwa na ushindani mkubwa kutoka katika mitandao mingine ikiwemo Twitter. 

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
26 Jul, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
27 Jul, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
27 Jul, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Hizi ndio passport 5 zenye nguvu zaidi duniani

Hizi ndio passport 5 zenye nguvu zaidi duniani

Nukta TV

Hii ndio spirulina: Hazina ya maji inayoboresha afya za Watanzania

Hii ndio spirulina: Hazina ya maji inayoboresha afya za Watanzania

Nukta TV

Mradi wa Sh4.6 bilioni kutoa ahueni ya umeme Lindi, Mtwara

Mradi wa Sh4.6 bilioni kutoa ahueni ya umeme Lindi, Mtwara

Nukta TV