Boniface Jacob afikishwa Mahakama ya Kisutu

September 19, 2024 5:24 pm · Fatuma Hussein
Share
Tweet
Copy Link
  • Afikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam.

Dar es Salaam. Meya wa zamani wa Ubungo na kada wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Boniface Jacob maarufu kama ‘Boni Yai’ amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Kazi Kisutu Dar es salaam leo Septemba 19,2024.

 Boni Yai amefikishwa mahakamani hapo ikiwa ni siku moja baada ya kukamatwa na Jeshi la Polisi saa kumi jioni Septemba 18, 2024 akiwa maeneo ya Sinza.

Kwa mujibu wa Msemaji wa Jeshi la Polisi, David Misime katika taarifa aliyoitoa jana Septemba 18, 2024 alisema jeshi hilo limemkamata na linamshikilia Jacob, mkazi wa Mbezi Msakuzi, jijini Dar es Salaam kutokana na makosa ya kijinai anayotuhumiwa nayo.

Kwa mujibu wa Wakili wa Chadema Hekima Mwasipu aliviambia vyombo vya habari kuwa polisi walimkamata Jacob na kufanya upekuzi wa takriban saa tatu nyumbani kwake.

Kukamatwa kwa Boni Yai kumezua mijadala katika mitandao ya kijamii ambapo kumekuwa na mashinikizo ya kutaka afikishwe mahakamani kusomewa mashtaka yanayomkabili kwa mujibu wa sheria.

Aidha, Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu(LHRC) kupitia mtandao  wa X zamani Twitter kimetoa wito kwa vyombo vya usalama kuhakikisha mashtaka dhidi ya Jacob yanakuwa wazi, na kwamba uchunguzi ufanywe kwa uwazi huku sheria zikizingatiwa.

Masoko & Zaidi
Loading…
No recent matches
No upcoming matches
/
No matches found for this filter
15 Jun, 2026 · TZS
No forex gainers today
No forex losers today
Forex rates unavailable
15 Jun, 2026 · TZS
No gainers today
No losers today
15 Jun, 2026
No active movers today

Inaendeshwa na Nukta AI

Follow us on TikTok

Nukta Habari

FOLLOW NOW
Subscribe to our channel

Nukta TV

SUBSCRIBE NOW
Mwenendo wa deni la serikali

Mwenendo wa deni la serikali

Nukta TV

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Rais Samia: Uchumi wa nchi unapanda , lakini ukifika kwa watu hali si nzuri

Nukta TV

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Gavana Tutuba afichua kiasi cha dhahabu kilichopo BoT thamani yake

Nukta TV